Wagombea 7 walijisajili kugombea urais nchini Iran wameonyesha katika kampeni na midahalo ya uchaguzi kwamba, wote wanakutana katika nukta moja muhimu, nayo ni kufanya mageuzi katika mitazamo kwa kutumia fursa zilizopo, iwapo watahabatika kushinda nafasi hiyo.
Hadi kufikia Jumatano ambayo ilikuwa siku ya mwisho ya kufanya kampeni, wagombea waliokuwa wamesalia katika mchuano wa urais ni pamoja na Ebrahim Raisi, Mohsen Rezaei, AbdulNasser Hemmati na Amir-Hossein Ghazizadeh-Hashemi. Waliojiondoa katika mchuano wa urais mwaka huu ni pamoja na Mohsen Mehr-Alizadeh, Alireza Zakani, na Saeed Jalili. Rais wa sasa Hassan Rouhani ambaye anamaliza muhula wake wa pili mfululizo haruhusiwi kisheria kugombea awamu hii ya urais.
Upigaji kura umeanza saa moja asubuhi na utaendelea hadi saa sita usiku na iwapo kutakuwa na haja zoezo la upigaji kura linaweza kuongezwa.
Wananchi wanapiga kura kwa kuzingatia kanuni za kiafya za kuzuia maambukizi ya COVID-19.
Kwa mujibu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Iran zaidi ya Wairani 59.3 wametimiza masharti ya kupiga kura katika uchaguzi wa Ijumaa ambapo mbali na kumpigia kura rais, wapiga kura pia watawachagua wajumbe wa mabaraza ya Kiislamu ya miji na vijiji.