Katika mkutano huo uliofanyika kwa njia ya video, wawili hao pia walisisitiza kuwa janga la COVID-19 limeonyesha kuna haja ya hatua za pamoja na ushirikiano wakati wa maafa.
El-Tayeb amebainisha uungaji mkono wake kwa pendekezo la Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ambaye amependekeza usitishwaji vita katika maeneo yote ya vita na uungaji mkono wa wakimbizi walioathiriwa na janga la corona.
Welby kwa upande wake amepongeza uhusiano wa kistratijia baina ya Al-Azhar na Canterbury na kusema na kusema mazungumzo ya amani baina ya pande mbili ni yenye manufaa na yamekuwa na taathira hasa kwa vijana.