"Ujenzi wa misikiti mipya unalenga kwenda sambamba na ukuaji wa idadi ya watu nchini na upanuzi wa miji," Ahmed Toufiq alisema wakati wa maadhimisho ya Siku ya Misikiti katika mji mkuu wa Morocco wa Rabat.
Wizara yake inataka kujenga "misikiti 80 katika miaka mitano ijayo," aliongeza, akitoa wito kwa wafadhili "kuunga mkono serikali katika kujenga misikiti 1,000 katika kipindi hicho cha miaka mitano."
"Kwa sasa kuna jumla ya misikiti 2,216 iliyofungwa, 723 kati yake iko katika mchakato wa ukarabati ili kufunguliwa," Toufiq alidokeza.
Kuna misikiti 51,000 nchini Morocco, asilimia 72 ambayo iko mashambani, waziri huyo alibainisha.
3480933