Khalid Mashal Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu wa Palestina Hamas amesema kuwa, usitishaji wowote wa vita unapaswa kufungamana na uondoshwaji mzingiro wa kidhuluma uliowekwa dhidi ya wananchi wa Ghaza.
2014 Aug 11 , 18:30
Waislamu wa jamii ya Rohingya nchini Myanmar wangali wanaishi katika hali ngumu na mazingira mabaya na makumi ya maelfu miongoni mwao wanakabiliwa na uhaba wa chakula, maji na huduma za afya.
2014 Aug 09 , 16:46
Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Waislamu katika Ukanda wa Ghaza hatimaye watapata ushindi dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel na kwamba Iran daima itasimama pamoja mataifa yote yanayodhulimiwa wakiwemo Wapalestina, Wairaqi na Wasyria.
2014 Aug 06 , 21:24
Makubaliano ya muda ya usitishwaji vita yameanza kutekelezwa katika Ukanda wa Ghaza baada ya utawala ghasibu wa Israel kulazimika kukubali masharti ya wanamapambano wa Kipalestina ya kuondoa majeshi yake katika ukanda huo.
2014 Aug 06 , 17:29
Jeshi la utawala haramu wa Israel limeendeleza mauaji ya umati katika eneo la Ukanda wa Ghaza hii leo kwa siku ya 28 mtawalia na kuifanya idadi ya mashahidi wa hujuma hiyo kukaribia 2,000.
2014 Aug 04 , 19:31
Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuendelea kimya na kutojali Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa UNSC ndio chanzo kikuu ambacho kimeufanya utawala wa Kizayuni wa Israel uendelee kupata kiburi cha kuendeleza jinai zake dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza.
2014 Aug 04 , 16:58
Utawala wa Kizayuni wa Israel haujatosheka kwa kuwaua kwa umati wanawake na watoto wa Ghaza bali pia umeharibu kwa mabomu idadi kubwa ya misikiti na mahospitali katika ardhi hiyo ya Wapalestina.
2014 Aug 03 , 10:12
Huku utawala wa Kizayuni wa Israel ukiendeleza jinai za kivita na mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina wasio na ulinzi wala hatia huko katika Ukanda wa Ghaza, Marekani imejitokeza wazi kuunga mkono kwa hali na mali jinai za utawala huo bandia.
2014 Aug 02 , 19:48
Duru za habari katika Ukanda wa Ghaza zinaarifu kuwa, karibu Wapalestina 1,700 wameshauawa shahidi katika jinai za siku 27 mtawalia za utawala huo katili wa Kizayuni kwenye ukanda huo.
2014 Aug 02 , 19:40
Banki ya KCB (Kenya Commercial Bank) nchini Kenya imetangaza kuwa itaanzisha rasmi mfumo kamili wa Kiislamu katika huduma za banki mwezi wa Agosti huku ikipanga kueneza huduma hiyo katika eneo lote la Afrika Mashariki.
2014 Jul 31 , 13:25
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuwa, 'ulimwengu wa Kiislamu kwa kuweka kando hilitalfu zilizopo, utumie uwezo wake wote kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza.'
2014 Jul 29 , 19:57
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kwamba, ulimwengu wa Kiislamu unapasa kuipatia kipaumbele kikubwa kadhia ya Ghaza.
2014 Jul 29 , 19:51
Baadhi ya Waislamu katika nchi za Iraq, Uturuki, Qatar, Misri, Saudi Arabia na Bahrain leo wanasherehekea sikukuu ya Idul Fitr baada ya kutangazwa rasmi mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani katika nchi hizo.
2014 Jul 28 , 12:09